MULUGO AOMBA RADHI KWA YALIYOTOKEA

Siku chache mara baada ya Naibu waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi  Philipo Mulugo kudaiwa  kubolonga alipokuwa akiwasilisha hotuba yake katika mkutano  wa kimataifa kwa kuonyesha mbele ya jamii ya kimataifa kuwa haijui historia ya nchi yake naibu huyo amewaomba radhi watanzania.

Akizungumza katika kipindi cha power break fast kinachorushwa  na kituo cha redio clous cha jijini Dar es salaam leo  kwa njia ya simu kutokea Dodoma mulugo alisema kuwa maelezo hayo yalitokana na kuchanganya jina la Zimbabwe na Zanzibar” kwanza niombe msamaha kwa yaliyotekea huko unajua ndugu mtangazaji kuna maneno mengi yamesemwa mara eti  sijui kingereza mara sijui historia ya nchi lakini ukweli ni kwamba nilipoenda kuwasilisha hotuba yangu kuna mjumbe kutoka Zimbabwe alikuwa amemaliza kuongea kama dakika mbili tu sasa wakati mimi nikawa nachanganya Zimbabwe na Zanzibar kwa sababu herufi zake zinaanzia na z “ alisema mulugo.

Alipotakiwa kueleza juu ya kukosea mwaka wa kuzaliwa Tanzania  naibu waziri huyo alisema kuwa hiyo inatokana na kuteleza kwa ulimi kwani historia ya cchi hata mtoto wa darasa la pili anaijua” kuna kitu kina itwa lang sleep  wakati nataja mwaka nilikosea nikaongeza namba badala ya kutaja moja nikataja moja moja mbili, mimi nimesoma historia  na uchumi na niliwahi kuwa mwalimu nimefundisha wanafunzi wengi sana  huwezi kusema hata mwaka wa kuzaliwa Tanzania siujui wakati hata mtoto wa darasa la pili anaujua” aliongeza mulugo

Dhahama hiyo imemkumba naibu waziri huyo  wakati akiwasilisha mada yake katika mkutano wa viongozi wa Afrika na taaluma ya elimu uliofanyika nchini  Aafrika ya kusini, Naibu huyo aliwambia wajumbe hao kuwa Tanzania ilizaliwa mwaka 11964 kutokana na muunganiko  wa visiwa  viwili pemba na Zimbabwe, kitu kilichoibua maswali mengi miongozi mwa watanzania juu ya uelewa wa naibu huyo na elimu yake kwa ujumla.

1 Comment

  1. habari24 said,

    October 26, 2012 at 4:34 pm

    yes


Leave a comment